Tarehe 02 Oktoba 2025, Mhe. Balozi Iddi Seif Bakari alifanya mazungumzo na Bw. Deodat Maharaj, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Teknolojia (United Nations Technology Bank) lenye Makao yake Makuu jijini Ankara, Uturuki. Katika mazungumzo hayo walijadili mkakati wa Shirika hilo unaolenga kuimarisha matumizi teknolojia nchini Tanzania kwenye sekta za kipaumbele ikiwemo kilimo, biashara na shughuli za uvuvi endelevu hususan kilimo cha mwani nchini ili kukuza ushiriki wa sekta wa sekta binafsi na kuongeza mchango wa sekta hizo kwenye uchumi na kuinua maisha ya wananchi.